HABARI
Rais Magufuli awajibu wanaokosoa mpango wa walimu wa sekondari kupelekwa shule ya msingi
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli amewajibu watanzania ambao wanakosoa mpango wa serikali wa kuwapeleka walimu wa sekondari kufundisha shule ya msingi.
Rais
Magufuli amesema kuwa kitendo hicho ni cha kawaida kwani hakiadhiri
mishahara yao bali kinawapa muda mwingi walimu hao kufanya kazi nyingine
za ziada.
“Wakati wa Nyerere walikuwa wanachukuliwa walimu wa UPE kwenda kufundisha shule za msingi. Sasa tunachukua wenye digrii.
"Kikubwa kinachoangaliwa ni mshahara wake tu.. Kwa sababu mshahara unapimwa si kwa vile unafundisha shule ya msingi, ni kutokana na Qualification zako.
"Tena kule ni kurahisi tu unaweza kufanya na mambo yako mengine.“alisema Rais Magufuli jana Mei 2, 2018 wakati akizungumza na wafanyakazi na wanafunzi wa Chuo Kikuu Kishiriki cha Elimu Mkwawa, kilichopo mkoani Iringa.
"Kikubwa kinachoangaliwa ni mshahara wake tu.. Kwa sababu mshahara unapimwa si kwa vile unafundisha shule ya msingi, ni kutokana na Qualification zako.
"Tena kule ni kurahisi tu unaweza kufanya na mambo yako mengine.“alisema Rais Magufuli jana Mei 2, 2018 wakati akizungumza na wafanyakazi na wanafunzi wa Chuo Kikuu Kishiriki cha Elimu Mkwawa, kilichopo mkoani Iringa.
Rais
Magufuli alitolea mfano wa nchi zinazotumia Maprofesa kufundisha shule
ya msingi; “Ukienda nchi za Scandinavia utakuta maprofesa ndiyo
wanafundisha chekechea, na mishahara yao ni mikubwa kuliko wanaofundisha
chuo kikuu. Just mind set.”
Mwezi
Februari mwaka huu serikali kupitia Ofisi ya Rais, Menejimenti ya
Utumishi wa Umma ilitangaza kuwa baadhi ya walimu wa masomo ya sanaa
kutoka shule za sekondari watapelekwa shule za msingi ili kukidhi
mahitaji.
WAZIRI ASEMA SI KILA MTU ANA MAMLAKA KUAGIZA UPIMAJI DNA
Kwa mujibu wa taarifa ya Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano UDART, Deus Bugaywa ambayo imesambazwa kwa vyombo vya habari na mitandao ya kijamii, maji yamejaa katika eneo la Jangwani na kupita juu ya Daraja la Mto Msimbazi. Mkuu huyo amewataarifu wateja wa huduma hiyo ya usafiri kuwa maeneo mengine ya jiji la Dar es Salaam yanaendelea kupata huduma ya mabasi ya UDART kama kawaida kwa kuwa mvua hazijasababisha athari sehemu hizo.
“Kwa sasa huduma zinatolewa kwa njia za Mbezi-Kimara, Kimara-Morocco, Kimara-Magomeni Mapipa, Kivukoni-Muhimbili, Gerezani-Kivukoni na Gerezani-Muhimbili. Huku taarifa hiyo ikuomba radhi wateja kutokana na usumbufu uliojitokeza, UDART imewahakikishia kuwa huduma hizo zitarejea pindi barabara itakapofunguliwa.
WAZIRI ASEMA SI KILA MTU ANA MAMLAKA KUAGIZA UPIMAJI DNA
Serikali
imekataza Mamlaka ya Wakala wa Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali
(GCLA), kuruhusu watu au taasisi zisizo na mamlaka kisheria kuwaamuru
kupima sampuli za vinasaba (DNA).
Agizo hilo lilitolewa jana jijini Dar es
Salaam na Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na
Watoto, Dk. Faustine Ndugulile, katika hafla ya uzinduzi wa Bodi Tendaji
ya GCLA.
Bodi hiyo ina wajumbe saba kutoka Wizara
za Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto; Mambo ya Ndani ya
Nchi, Katiba na Sheria na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM).
Dk. Ndugulile ameitaka mamlaka hiyo
kutoa elimu kwa jamii kuhusu majukumu ya mamlaka hiyo, ili kuepuka watu
au taasisi kutoa maagizo juu kwa mamlaka hiyo kinyume cha sheria na
taratibu.
“Tusiamini kila mtu anajua utaratibu.
Tunaweza sasa kuja kuvumbua mambo ambayo hayapo. Si kila mtu anaweza
kuamrisha Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali kuchukua vipimo
vya DNA, si hivyo kuna taratibu zake,” alisema.
Alisema lazima watu waelezwe taratibu
zikoje, nani anawajibika kwenda kupeleka sampuli na nani ana wajibu huo
kwa sababu majukumu yake ni ya kisheria.
Dk. Ndugulile alisema katika siku za
karibuni suala la kupima vinasaba limezungumziwa sana hali ambayo imezua
mkanganyiko kwa jamii, hivyo kuitaka mamlaka hiyo kutimiza wajibu wa
kutoa elimu.
Pamoja na kutokumtaja mtu aliyetoa amri
ya watu kupimwa DNA, hivi karibuni Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul
Makonda, aliwaita watu waliodaiwa kutelekeza watoto kujitokeza.
Baadhi ya watu hao walijitokeza, lakini
90 kati ya wanaume hao, waliwakana watoto waliodaiwa kuwa wamewatelekeza
na kutaka waende wakapimwe DNA katika maabara ya Mkemia Mkuu ili
kumaliza utata huo.
Katika hatua nyingine, Dk. Ndugulile
aliitaka taasisi hiyo kuwa na mkaguzi wa kimataifa wa ubora wa sampuli
wanazopima, ili zikubalike kitaifa na kimataifa.
“Lazima muwe na mkaguzi wa kimataifa wa
kuthibitisha kile mlichopima kwa sababu taasisi hii ina majukumu ya
kisheria ya kuamua ukweli kuhusu sampuli iliyopimwa. Mkisema huu ni unga
wa mahindi ilhali tunaona ni dawa za kulevya hatuwezi kupinga,”
alisema.
Pia aliitaka mamlaka hiyo kutoa majibu
kwa wakati, ili kupunguza kesi zilizopo mahakamani zinazosubiri majibu
ya maabara hayo.Alisema, ili kutekeleza agizo hilo, amewataka kuandaa
mikataba inayoonyesha kazi itakamilika kwa muda gani pindi wanapopokea
sampuli.
“Utakumbuka kuna wakati kesi
zilirundikana katika mahakama zetu hivyo mnatakiwa kufanya kazi kwa
haraka na kwa wakati na muwe na mikataba inayoonyesha kazi itakamilika
kwa muda gani,” alisema.
Pia aliwataka kuwatambua wale wote
wanaojihusisha shughuli za kemikali nchini wakiwamo, wauzaji, wanunuzi
na wanaozitumia kwa ajili ya kupunguza matukio ya uhalifu nchini.
Kadhalika aliwataka kushirikiana na
Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi na Mazingira (NEMC) kuthibiti
majitaka katika viwanda, ili kuepusha madhara kwa watu.
“Sijawasikia mkipima maji taka
yanayotiririka viwandani mmekaa kimya kama si wajibu wenu, hakikisheni
mnashirikiana nao na kuchukua sampuli nyie wenyewe mpime na mtoe
majibu,” alisema.
Naye Mkemia Mkuu wa Serikali, Dk.
Fidelice Mafumiko, alisema GCLA inakabiliwa na uhaba wa watumishi
takribani 200 na pia uchakavu wa mitambo ya kimaabara.
Dk. Mafumuko pia alisema fedha za bajeti
ya serikali ya mwaka 2017/18 zilizotengwa kwa ajili ya kununua mitambo
na vifaa vya maabara hiyo hazijatoka hadi sasa hali ambayo inawafanya
kushindwa kutekeleza majukumu yako kikamilifu.
Naye Mwenyekiti wa Bodi hiyo, Prof.
Ester Jason, aliahidi kuisumbua wizara hiyo kuhusu kutekeleza majukumu
ya mamlaka ikiwa ni pamoja na kutoa fedha mapema iwezekanayo.
Mafuriko yakwamisha ‘Mwendokasi’ Dar
Kampuni ya mabasi yaendayo haraka jijini Dar es Salaam (UDA-RT) imesitisha huduma ya usafiri kuanzia saa sita mchana leo, Ijumaa, baada ya Barabara ya Morogoro kufungwa eneo la Jangwani ambalo limefurika kutokana na mvua zinazoendelea kunyesha.Kwa mujibu wa taarifa ya Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano UDART, Deus Bugaywa ambayo imesambazwa kwa vyombo vya habari na mitandao ya kijamii, maji yamejaa katika eneo la Jangwani na kupita juu ya Daraja la Mto Msimbazi. Mkuu huyo amewataarifu wateja wa huduma hiyo ya usafiri kuwa maeneo mengine ya jiji la Dar es Salaam yanaendelea kupata huduma ya mabasi ya UDART kama kawaida kwa kuwa mvua hazijasababisha athari sehemu hizo.
“Kwa sasa huduma zinatolewa kwa njia za Mbezi-Kimara, Kimara-Morocco, Kimara-Magomeni Mapipa, Kivukoni-Muhimbili, Gerezani-Kivukoni na Gerezani-Muhimbili. Huku taarifa hiyo ikuomba radhi wateja kutokana na usumbufu uliojitokeza, UDART imewahakikishia kuwa huduma hizo zitarejea pindi barabara itakapofunguliwa.
Comments
Post a Comment